Posts

Showing posts from August, 2015

Msimamo wa ligi kuu uingerza mara baada ya mechi za jana

Image

VERMAELEN APELEKA USHINDI BARCELONA

Image
MABINGWA watetezi, Barcelona wamepata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Malaga Uwanja wa Camp Nou katika mchezo wa La Liga. Shukrani kwake mfungaji wa bao hilo pekee, beki Mbelgiji Thomas Vermaelen dakika ya 73. Mbelgiji huyo alikuwa nje kwa majeruhi karibu mwaka mzima msimu uliopita baada ya kusajiliwa kutoka Arsenal. Luis Suarez, Lionel Messi na Neymar wote walianza katika safu ya ushambuliaji, lakini hakuna kati yao aliyefumga.  Kikosi cha Barcelonakilikuwa Bravo; Sergi Roberto, Mascherano, Vermaelen, Alba/Mathieu dk89, Busquets, Rakitic/Rafinha dk64, Iniesta, Messi, Suarez na Neymar/Sandro dk85. Malaga; Kameni; Rosales, Angeleri, Weligton/Albentosa dk25, Torres, Horta, Tissone, Recio; Juankar, Amrabat/Charles dk53

WAPENZI WA MAGUFULI,CCM,LOWASSA,UKAWA RATIBA NZIMA YA KAMPENI 2015 YA VYAMA VYOTE NCHI NZIMA ZA UCHAGUZI MKUU HII HAPA..ISOME USIPITWE

Image
Bonyeza hapa kuitazama ratiba hiyo

Kuhusu ubora wa Coquelin, Wenger amesema haya.

Image
Arsene Wenger amesisitiza kuwa kwa upande wa takwimu, Francis Coquelin moja ya viungo bora wa ulinzi barani Ulaya. Coquelin ametokea kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Arsenal katika miezi ya hivi karibuni,  kufuatia ujio wake kutoka klabu ya Charlton Athletic mwezi Desemba ambapo alikuwa akikipiga kwa mkopo. Mfaransa huyo ameshacheza michezo mitatu mikubwa ya ligi kuu Uingereza mpaka sasa msimu huu, lakini alikosolewa na machambuzi wa kituo cha Televisheni cha Sky Sports Gary Neville katika maandalizi ya mchez0 dhidi ya Liverpool, ambapo walitoka suluhu, lakini Wenger amemkingia kifua na kusema kinda wake huyo ni mchezaji maridadi. Kwa uhakika kabisa, Wenger anaamini kwa namna takwimu zinayoonesha, basi Coquelin ni mchezaji bora ulimwenguni katika nafasi yake. “Coquelin ana takwimu nzuri sana kwenye upande wa eneo kiungo wa ulinzi  barani Ulaya. Nadhani huwa mnaangalia mpira kama ambavyo huwa naangalia. Mimi sijui watu huwa wanaona nini...

cheki mapicha ya jangwani kwenye ufunguzi wa kampeni za ukawa

Image
picha na mpekuzi blog

NEC yaonya vyama vya siasa vitakavyokiuka ratiba za kampeni

Image
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, kuhakikisha vinafuata na kuheshimu ratiba ya uchaguzi waliyojiwekea. Katika taarifa kwa njia ya video iliyotumwa kwa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhani amesema kuwa vyama vyote vilishiriki katika kuandaa ratiba hiyo na kuwa viliiridhia hivyo hawana budi kuhakikisha wanaifuata. “Tulikaa na vyama, mimi sikuamua hii ratiba, wao walipendekeza na wakakubaliana na wakatoa ratiba hii, cha kwanza kabisa vyama vya siasa wazingatie waliyoyaweka humu,” alisema Kailima. Aliongeza kuwa utaratibu huo upo kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Uchaguzi ya 2015 na kuwa wakikiuka, sheria itawakamata. “Kwenye maadili (Sheria ya Maadili ya Uchaguzi 2015) kuna eneo ambalo vyama vya siasa na wagombea wanakubaliana kuzingatia muda wa kuanza kampeni na muda wa kumaliza kamp...

TOP TEN YA MASTAA WENYE FOLOWERS WENGI INSTAGRAM

Image
Kim Kardashian amevunja rekodi ya msanii Beyoncé kwa kuwa na followers wengi zaidi instagram, mpaka sasa Kim K amepata followers milioni 44. Kim kapata watu hawa ndani ya siku chache baada ya kutangza kutegemea mtoto wa pili na kuonyesha mabadiliko ya mwili wake. Hii ndio top ten ya mastaa wenye followers wengi zaidi duniani. 1. Kim Kardashian — 44,005,604 2. Beyoncé — 43,935,648 3. Taylor Swift — 43,533,226 4. Selena Gomez — 41,843,095 5. Ariana Grande — 41,696,873 6. Justin Bieber — 36,994,254 7. Kendall Jenner — 35,388,483 8. Kylie Jenner — 33,703,166 9. Nicki Minaj — 32,278,123 10. Khloé Kardashian — 30,522,261

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMIS 20.08.2015

Image
Bayern Munich wamewaambia Manchester United kuwa kiungo Thomas Muller, 25 hauzwi, kufuatia taarifa kuwa wametoa dau la pauni milioni 60 (Manchester Evening News), Manchester United pia wamepata pigo jingine baada ya Southampton kusema hawamuuzi mshambuliaji wao Sadio Mane, 23 (Daily Star), Real Madrid wamekubali dau la pauni milioni 43 kutoka kwa Arsenal ili kumsajili Karim Benzima (Talksport), Wolfsburg watamuuza kiungo wao Kevin De Br yne, 24, kwenda Manchester City iwapo klabu hiyo itatoa pauni milioni 57 (Daily Mirror), West Ham wamejitoa katika kumfuatilia Emmanuel Abebayor kutoka Tottenham (Telegraph), West Brom wanajaribu kumsajili Federico Fazio, 28, kutoka Tottenham (Daily Mirror), mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge, 25, anatarajiwa kurejea Anfield mwishoni mwa wiki baada ya kukamilisha matibabu yake nchini Marekani, na huenda akacheza mechi yake ya kwanza, Septemba 12 dhidi ya Manchester United (Guardian). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!  ...

Ratiba ya ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2015/2016 hii hapa

Image
Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) imetoka leo ambapo jumla ya timu 16 zinashiriki ligi hiyo itakayoanza kutimua vumbi Septemba 12 katika viwanja tofauti nchini na kumalizika Mei 7, 2016.  Ifuatayo ni ratiba nzima ya michuano hii…..   Round 1 12.09.2015(Sat) 1 NDANDA FC Vs MGAMBO SHOOTING NANGWANDA MTWARA 12.09.2015(Sat) 2 AFRICAN SPORTS Vs SIMBA SC MKWAKWANI TANGA 12.09.2015(Sat) 3 MAJIMAJI FC Vs JKT RUVU MAJIMAJI RUVUMA 12.09.2015(Sat) 4 AZAM FC Vs TANZANIA PRISONS AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM 12.09.2015(Sat) 5 STAND UNITED Vs MTIBWA SUGAR KAMBARAGE SHINYANGA 12.09.2015(Sat) 6 TOTO AFRICANS Vs MWADUI CCM KIRUMBA MWANZA 12.09.2015(Sat) 7 MBEYA CITY Vs KAGERA SUGAR SOKOINE MBEYA 13.09.2015(Sun) 8 YOUNG AFRICANS Vs COASTAL UNION NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM  Round 2 16.09.2015(Wed) 9 YOUNG AFRICANS Vs TANZANIA PRISONS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM 16.09.2015(Wed) 10 MGAMBO SHOOTING Vs SIMBA SC MKWAKWANI TANGA 16.09.2015(Wed) 11 MAJIMAJI FC...