Posts

Showing posts from May, 2017

Tiger Woods -Sikuwa nimelewa kwa kunywa pombe

Image
Mcheza gofu maarufu duniani  Tiger Woods,  amesema hakuwa amekunywa pombe alipokamatwa akiendesha gari jimbo la Florida mapema hapo jana. Mchezaji huyo alifunguliwa mashtaka ya kuendesha gari akiwa amelewa, lakini amesema ulevi wake ulitokana na dawa alizokuwa amezinywa kwa ushauri wa daktari. Polisi wa Palm Beach County,Forida,  wamempiga picha akionekana kuwa mchovu na nywele zikiwa rafu. “Nafahamu uzito wa kitendo nilichokifanya na nawajibika kikamilifu na vitendo vyangu,” alisema. Polisi walitoa picha ya Bw Woods,  akionekana kutokuwa  nadhifu,  nywele zake zikiwa hazijachanwa  na macho akiwa ameyatoa nje na kuonekana mwenye uchovu. Alikamatwa katika mji wa Jupiter. “Nataka umma ufahamu kwamba pombe haikuhusika kwa vyovyote vile. Kilichotokea ni madhara ambayo hayakutarajiwa ya kutumia dawa kwa ushauri wa daktari,” alisema. “Sikugundua kwamba kuchanganya dawa kungeniathiri sana hivyo.” Aliongeza, “Ningependa kuomba radhi ...

YALIYOJIRI LEO BUNGENI MJINI DODOMA

Image
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Najma Giga akiongoza kikao cha 37 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 30, 2017.  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 37 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 30, 2017.  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Mbunge wa Kaliua(CUF) Mhe.Magdalena Sakaya katika kikao cha 37 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 30, 2017.   Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe,Prof.Joyce Ndalichako akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 37 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 30, 2017.  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angelina Kairuki akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 37 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjin...

Maneno ya mzee akilimali baada ya manji kujiuzulu

Image
Katibu wa baraza la wazee wa Yanga Mzee Ibrahim Akilimali amesema, huenda kujiuzulu kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji ni kutikisa kibiriti tu lakini atarejea tena kwenye nafasi yake kwa sababu tayari alishawahi kutangaza kujiuzulu halafu akarejea baada ya kuombwa na wanachama kufanya hivyo. Mzee Akilimali amesema mara ya kwanza Manji alipotangaza kujiuzulu alitukanwa na kutishiwa maisha hadi kutaka kuchomewa nyumba yake lakini baadae Manji alirejea kwa hiyo bado haamini kama amejiuzulu jumla au anatikisa kiberiti kama mwanzo. “Mimi siamini kwa sababu mguu uliomumwa na nyoka ukikanyaga jani unaogopa, aliposema anajiuzulu basi nilitishiwa amani kabisa na kutukanwa matusi ya laana siwezi kuzungumza nikawa naishi kwa kibali cha polisi ili kunipa usalama lakini alikuwa anatishia, pengine na wakati huu anatishia,” amesema Akilimali wakati akihojiwa na kituo cha EFM Radio. “Wana Yanga wawe wavumilivu wawe na utulivu kwa sababu hatima tutaisikia kwa sababu mimi nashin...