RASMI, HUKUMU Ya DMX Imetajwa, Ni KIFUNGO cha….

TMZ imeripoti Legend wa HipHop DMX anarudi jela kutumikia kifungo cha mwaka mmoja kwa kosa la kukwepa kodi ya dola milioni 1.7 katikati ya mwaka 2002 na 2005,
Upande wa mashtaka uliomba afungwe miaka mitano jela ili iwe funzo kwa wasanii wengine wanaopenda kukwepa kodi, awali alitakiwa kufungwa miaka 40 jela.
Wakili wa DMX , Murray Richman alicheza muziki wa DMX mahakamani, wimbo “Slippin” ili jaji aelewe ugumu wa maisha aliopitia DMX Na ndio kilichopelekea staa huyu kupunguziwa adhabu.
Mahakamani jana Jiji Jed Rakoff  alisema  DMX ‘ni mtu mzuri anayefanya makosa makubwa kwenye maisha yake, yeye mwenyewe ndio adui yake namba moja’

Comments

Popular posts from this blog

Pichaz za matukio yaliyo jiri magufuli alipokuwa chato leo

Crystal Palace kuivaa Man united –FA CUP