RONALDO AMZUNGUMZIA MAMA WA MWANAE PAMOJA NA KURUDI MAN UNITED
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Ronaldo amesema hatomtaja mama wa mtoto wake mpaka atakapoona muda umefika
Mchezaji Cristiano Ronaldo wa Real Madrid, amesema kamwe hatomtaja
mama mzazi wa mtoto wake Ronaldo Jr. na kwamba muda ukifika atamuweka
wazi huku mwanae pia akitakiwa kusubiri muda muafaka apate kumjua mama
yake.
Amesema kuwa amekua akishiriki mapenzi na warembo tofauti tofauti
huku akikiri kuwa hiyo sio yeye tu bali ni tatizo kwa nyota wengi
duniani kupitia maisha hayo huku akijinasibu kuwa kwasababu yeye ni
mrefu, mwenye mwili mzuri wa mazoezi basi huwamaliza akina dada. Ronaldo ameweka wazi maisha yake binafsi wakati akifanyiwa mahojiano na Jonathan Ross
Kuhusu Balon d’Or msimu huu, Ronaldo anasema Messi atatwaa tuzo hiyo
kutokana na klabu yake ya Barcelona kutwaa makombe yote matatu
iliyoshiriki msimu uliopita. Huku Ronaldo akisema ulikua ni msimu mzuri
zaidi kwake binafsi kutokana na kufunga magoli mengi katika kila
mashindano.
Ronaldo ambaye alikua jijini London kwa utambulisho wa filamu yake ya
maisha yake ya soka, anasema kamwe hatarajii kustaafu hivi karibuni
huku akisema atamaliza mpira wake katika ligi bora na sio Marekani wala
Qatar. Huku akisema lolote linawezekana kwa yeye kirejea Manchester
United siku moja na kwamba tusubiri kuona.
Mchezaji
wa kimataifa wa Ureno Cristiano Ronaldo aliachana na penzi wake wa
zamani Irina Shayk aada ya kudumu kwenye uhusiano kwa miaka mitanosource shaffih dauda.com
Serikali imetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la 7 kwa mwaka 2016 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema ya mkoani Shinyanga ====>> Bofya << HAPA>> Kuyaona matokeo AU ===> Waweza Bofya pia <<HAPA>> Kuyaona
Msafara wa mgombea wa urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli ukielekea kwenye uwanja wa michezo Chato maarufu kama Mazaina. Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa michezo wa Mazaina Chato tayari kuhutubia wakazi wa Chato. Umati wa wakazi wa Chato wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya mkutano kwa ajili ya kumsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli. Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Joseph Musukuma na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Alhaji Abdallah Bulembo. Hii ndio meza kuu. Shilole akitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za CCM Chato Chege na Temba wakitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za Chato CCM. Mr.Blue akiwapagaisha wakazi wa Chato kwenye mkutano wa kampeni. Original Komedi wakitumbuiza wakazi wa Chato kwenye mkutano wa kampeni za CCM. Joti akipeana mkono na Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli ...
Klabu ya soka ya crystal Palace imetinga hatua ya Fainali ya FA CUP baada ya kuifunga Watford United Bao 2-1 kwenye Nusu Fainali. Kwa matokeo hayo ya mchezo huo uliochezwa Uwanjani Wembley, Jijini London, sasa Palace watakutana na Manchester United ambao waliwatoa Everton 2-1 katika Nusu Fainali nyingine. Hadi Mapumziko Palace walikuwa mbele kwa Bao 1-0 lililofungwa na Yannick Bolasie. Kipindi cha Pili, Watford walimudu kusawazisha kupitia Deeney lakini Dakika 6 tu baadae Connor Wickham akafunga Bao la Pili na la ushindi kwa Palace. Fainali Michuano hii itachezwa Mei 21 hapo hapo katika dimba laaWembley
Comments
Post a Comment