Hispania, Uingereza zaua kufuzu EURO,matokeo mengine haya hapa

Michuano
ya kuwania kufuzu kucheza Euro 2016 imeendelea kwa michezo kadhaa
kupigwa katika viwanja mbalimbali, moja kati ya mechi zilizochezwa usiku
wa Oktoba 9, timu ya taifa ya Uingereza ilikuwa mwenyeji wa timu ya
taifa ya Estonia.

Mechi
ambayo ilikuwa ngumu kwa Uingereza kuweza kupata nafasi ya kufunga goli
kutokana na timu ya taifa ya Estonia kuwa imejiandaa vyema kuwakabili
waingereza hao, uwezo wa kuhimili mashambulizi ya Waingereza ulidumu kwa
dakika 44 kabla ya dakika ya 45 Theo Walcott kupachika goli la kwanza
na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli 1-0 dhidi ya Estonia.

Uingereza
walirudi uwanjani kipindi cha pili wakiwa na faida ya goli moja kitu
ambacho kiliwapelekea Estonia kujaribu kutafuta nafasi ya kusawazisha
goli hilo ila Raheem Sterling aliwakatisha tamaa ya kusawazisha goli
hilo ambalo lingeweza kuwafanya waondoke na Point moja, Sterling
alipachika goli la pili dakika ya 85 ya mchezo na kufanya mechi
imalizike kwa Uingereza kuibuka na ushindi wa goli 2-0.

Comments
Post a Comment