Maamuzi ya UKAWA baada ya chama pinzani kukiuka taratibu za kisheria…

Suala
la uchaguziMkuu bado linagonga vichwa vya habari hapa nchini ambapo
Mwanasheria wa CHADEMA ambaye ni mkuu wa idara ya Uchaguzi kwenye
sheria,Bw.John Mallya jana alifanya mkutano wa kuzungumza na waandishi
wa habari kuhusu uki ukwaji wa sheria na chama pinzani.
Akizungumza
mbele ya waandishi wa habari Mallya alisema: "Ndugu waandishi wa habari
tumewaita hapa hususani mambo ya kisheria yanayoendelea kwenye kampeni
zoezi la uchaguzi ni zoezi la kikatiba, sheria ya uchaguzi wa taifa
mwaka 1985 kanuni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na maadili ya uchaguzi
wa Ubunge, Urais na Udiwani pamoja na sheria nyingine ikiwemo ya rushwa
na sheria ya vyama vya kisiasa".
‘Sheria
kwa mfano, ambayo ni maadili ya Uchaguzi ya mwaka huu vyama vyote
vinavyoshiriki uchaguzi huu kupitia makatibu wake wakuu wameweka saini
zao inakataza suala la mtu kutoa bango la mtu mwingine lakini chadema
imepata hiyo changamoto kwamba mabango yake wameondolewa kwa mfano hili
bango lipo Nyerere Road pale Mwanza limeondolewa na watu wa CCM ilikuwa
ni nyumba ya mtu binafsi wakamtishia watachoma nyumba yake wakamrushia
mawe wakavunja vioo vyake na baada wakaliondoa"
‘Na
hii inaonesha sio tu ni namna gani CCM wamekiuka sheria lakini hawafai
kutawala nchi kwasababu suala la kuweka bango ni suala la kisheria
ukiona bango la Samia,Magufuli na mtu yoyote limewekwa kisheria",
aliongeza Mallya.
‘Mabango,
sera, vipeperushi vyote vinakuwa vimesajili na tume ya Uchaguzi kwa
madhumuni ya Kampeni kwa mfano ujumbe wa Mabadiliko umesajiliwa na nembo
ya CHADEMA pia imesajiliwa, sasa CCM wanakiuka sheria wamekopi na
kupesti, wanachukua ilani na sera zetu ambapo wamechukua nembo yetu M4C
ambayo sisi tunaita Movement 4 Change huku CCM wakiwa wanasema M4C ni
Magufuli 4 Change‘ – John Mallya
‘Katika
hili tumechukua hatua nzito kuliko hizi za mwanza maana yake hili sio
la kimadili hili ni uvunjwaji wa sheria, Chadema tunampeleka Magufuli
Mahakamani pamoja na bodi ya wadhamini wa chama cha Mapinduzi",
alisema.
Comments
Post a Comment