Juma Nyoso tena na stori ya udhalilishaji stori na picha viko hapa

Juma Nyoso akifanya tukio la udhalilishaji dhidi ya John Bocco msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara
Juma Nyoso akifanya tukio la udhalilishaji dhidi ya John Bocco msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara

Mchezaji na nahodha wa timu ya Mbeya City Juma Nyoso ameendelea kufanya vitendo ambavyo si vya kiungwana na vinavyohitaji kupingwa kwa nguvu zote kwenye soka si la Tanzania pekee bali duniani kote ambako mchezo huu unachezwa.
Nyoso amemfanyia kitendo cha udhalilishaji mchezaji na nahodha wa Azam FC John Bocco ‘Adebayo’ wakati wa mchezo wa timu ya Azam FC dhidi ya Mbeya City uliochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi ambapo Azam FC waliiibuka na ushindi wa goli 2-1.
Kitendo kilichofanywa na Juma Nyoso ni cha kulaaniwa na kupigwa vita kwasababu kinaharibu maana halisi ya mchezo wa soka ambao ni wa kistaarabu unaochezwa na waungwana wapenda amani lakini kwa beki huyu wa Mbeya City haiko hivyo.
Msimu uliopita Nyoso alimfanyia kitendo kama alichokifanya leo kwa John Bocco aliyekuwa mshambuliaji wa Simba kwa wakati huo Elius Maguri ambaye kwa sasa anakipiga Stand United ya Shinyanga. Mazingira ya matukio hayo mawili yanafanana kwa asilimia nyingi.
Beki huyo wa zamani wa Simba SC alifanya tukio hilo wakati mpira ukiwa umesimama kama ilivyokuwa kwa Maguri msimu uliopita. Tukio la kumdhalilisha Maguri lilipelekea Nyoso afungiwe kucheza mechi nane za ligi kuu Tanzania bara.
Nyoso akifanya tukio la udhalilishaji dhidi ya Elius Maguri msimu uliopita wakati Maguri akicheza kwenye klabu ya Simba SC
Nyoso akifanya tukio la udhalilishaji dhidi ya Elius Maguri msimu uliopita wakati Maguri akicheza kwenye klabu ya Simba SC

Comments

Popular posts from this blog

Pichaz za matukio yaliyo jiri magufuli alipokuwa chato leo

Crystal Palace kuivaa Man united –FA CUP