Juma Nyoso tena na stori ya udhalilishaji stori na picha viko hapa
Mchezaji na nahodha wa timu ya
Mbeya City Juma Nyoso ameendelea kufanya vitendo ambavyo si vya
kiungwana na vinavyohitaji kupingwa kwa nguvu zote kwenye soka si la
Tanzania pekee bali duniani kote ambako mchezo huu unachezwa.
Nyoso amemfanyia kitendo cha
udhalilishaji mchezaji na nahodha wa Azam FC John Bocco ‘Adebayo’ wakati
wa mchezo wa timu ya Azam FC dhidi ya Mbeya City uliochezwa kwenye
uwanja wa Azam Complex, Chamazi ambapo Azam FC waliiibuka na ushindi wa
goli 2-1.
Kitendo kilichofanywa na Juma
Nyoso ni cha kulaaniwa na kupigwa vita kwasababu kinaharibu maana halisi
ya mchezo wa soka ambao ni wa kistaarabu unaochezwa na waungwana
wapenda amani lakini kwa beki huyu wa Mbeya City haiko hivyo.
Msimu uliopita Nyoso alimfanyia
kitendo kama alichokifanya leo kwa John Bocco aliyekuwa mshambuliaji wa
Simba kwa wakati huo Elius Maguri ambaye kwa sasa anakipiga Stand United
ya Shinyanga. Mazingira ya matukio hayo mawili yanafanana kwa asilimia
nyingi.
Beki huyo wa zamani wa Simba SC
alifanya tukio hilo wakati mpira ukiwa umesimama kama ilivyokuwa kwa
Maguri msimu uliopita. Tukio la kumdhalilisha Maguri lilipelekea Nyoso
afungiwe kucheza mechi nane za ligi kuu Tanzania bara.


Comments
Post a Comment