Wenger aweka sawa kati yake na Ozil
Arsene
Wenger ameweka wazi mpango wake wa kumpa Mesut Ozil fursa ya kudumu
kucheza namba kumi kuanzia msimu ujao wa ligi kuu nchini Uingereza na
mashindano mengine.
Ozil,
ambaye tangu asajiliwe kutoka Madrid hajaonesha kiwango kilichotarajiwa
na wengi, atapewa nafasi hiyo ili kurudisha makali yake kama alivyokuwa
akifanya Madrid.
Nyota
huyo wa Ujerumani amekuwa mara kadhaa akichezeshwa nafasi tatu tofauti
na Wenger hali ambayo hata yeye mwenyewe alionekana kutofurahishwa nayo.

Mesut Ozil (katikati) atachezeshwa namba kumi ya kudumu msimu ujao wa EPL.


Comments
Post a Comment