Hamis Kiiza kama mfalme Simba:
HAMIS Kiiza amejikuta akipokewa kama mfalme na mashabiki wa Simba waliokuwa wamelizingira gari lake mara alipotua katika mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa TCC Chang’ombe, Dar es Salaam jana asubuhi.
Sambamba na kulizingira gari hilo dogo aina ya Luxes yenye nambari T 832CTU, mashabiki hao walichangishana fedha na kumpa Mganda huyo kama sehemu ya kuonyesha jinsi wanavyomkubali na kufurahia ujio wake Msimbazi.
Kiiza alifika uwanjani hapo saa 2:00 asubuhi akiwa pamoja na Waganda wenzake, Simon Sserunkuma na Jjuuko Murushid ambapo wakati wenzake hao wakijumuika na wenzao mazoezini, yeye alibaki ndani ya gari hilo na kuwafanya mashabiki kulizingira mara baada ya kumalizika kwa mazoezi.
Sambamba na kulizingira gari hilo dogo aina ya Luxes yenye nambari T 832CTU, mashabiki hao walichangishana fedha na kumpa Mganda huyo kama sehemu ya kuonyesha jinsi wanavyomkubali na kufurahia ujio wake Msimbazi.
Kiiza alifika uwanjani hapo saa 2:00 asubuhi akiwa pamoja na Waganda wenzake, Simon Sserunkuma na Jjuuko Murushid ambapo wakati wenzake hao wakijumuika na wenzao mazoezini, yeye alibaki ndani ya gari hilo na kuwafanya mashabiki kulizingira mara baada ya kumalizika kwa mazoezi.

Comments
Post a Comment