Habari njema kwa Chelsea kuhusu Falcao
Hatimaye
Radamel Falcao amesaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Chelsea na
ataungana moja kwa moja kujumuika na wenzake katika kipindi hiki cha
maandalizi kabla ya msimu mpya kuanza huku nchini Marekani (Pre-season)
Baba
na Mjomba wa Falcao wamethibitisha rasmi habari hizo kwa gazeti la The
Guardian kwamba, ni kweli Chelsea wamemsajili mshambuliaji huyo raia wa
Colombia.
Kwa
mujibu wa gazeti hilo ni kwamba, Falcao atakipiga kwa mkopo kwa mwaka
mmoja kama ilivyokuwa kwa Man United huku kukiwa na kipengele cha
kumsajili moja kwa moja endapo kiwango chake kitamridhisha kocha wake.
Lakini
kwa upande wao Chelsea, bado hawajatangaza rasmi kuhusu tukio hili la
usajili wa Falcao huku tetesi zikisema kuwa, makubaliano ya awali
yalikuwa ni FALCAO kupewa kitita cha mshahara wa Pauni 265,000 kwa wiki.

Lakini
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Chelsea zinadai kuwa, watakuwa
wakimlipa mshahara wa takriban pauni 180,000 kwa wiki huku ada ya
uhamisho wa mkopo ikidaiwa kuwa ni kiasi cha pauni milioni 4
Ikumbukwe
tu wakala wa Falcao Jorge Mendes pia ni wakala wa kocha wa Chelsea Jose
Mourinho, na Mourinho ameahidi kukirudisha upya kiwango cha Falcao
ambacho kimepotea ghafla hasa baada ya kukumbwa na majeraha ya muda
mrefu kabla kujiunga na Mashetani Weundu Manchester United msimu
uliopita.
Comments
Post a Comment