Ajali Morogoro: Wanne wafariki na 21 kujeruhiwa

Watu wanne wamefariki dunia  leo na wengine 21 kujeruhiwa  kufuatia basi aina ya Isuzu kugonga treni ya abiria  iliyokuwa ikienda bara katika kilomita 276/0 kati ya stesheni za Kimamba na Kilosa Mkoani Morogoro wilayani Kilosa majira ya saa 11:25 asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotoewa na ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Mhandisi Elia Mshana amesema basi hilo lenye namba za usajili T 837 CTM Isuzu Coaster linalomilikiwa na Feisal A. Khuwel wa Kilosa.
Taarifa kutoka eneo la tukio limefafanua kuwa waliofariki ni wanaume wawili, mwanamke mmoja na mtoto wa miaka minne. Kwa upande wa majeruhi, majeruhi 21 wako wanaume 14 na wanawake 7 ambao wanaendelea na matibabu katika Hospital ya Wilaya ya Kilosa.
Hata hivyo baada ya ajali treni ya abiria imeondoka katika stesheni ya Kilosa saa 3 asubuhi kuendelea na safari yake kwenda Bara.
Wanne wafariki katika ajali mkoani Morogoro.

Comments

Popular posts from this blog

Pichaz za matukio yaliyo jiri magufuli alipokuwa chato leo

Crystal Palace kuivaa Man united –FA CUP