hii ndio movie mpya ya jb bonge la bwana inayotarajiwa kuingia sokoni wiki ijayo

Muigizaji, mtayarishaji na muongozaji wa filamu, Jacob Stevephen aka JB anatarajia kuachia filamu mpya wiki ijayo iitwayo Mzee wa Swagga.
Filamu hiyo iliyotayarishwa chini ya kampuni ya Jerusalem Film imeigizwa na wasanii mahiri akiwemo JB, Cassie Kabwita, Wastara, Wellu Sengo, Thea Mike, Ndubagwe Misayo na wengineo.
Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram aliwahabarisha mashabiki na kuandika; ‘MZEE WA SWAGA ITAKUWA MTAANI WIKI IJAYO’– aliandika @jb_jerusalemfilms

Comments
Post a Comment